Pages

Wednesday, April 30, 2014

SOMA HABARI KWA UFUPI



Watu 18 wamefariki dunia, wakiwemo polisi wanne na viongozi wote wa kijiji katika ajali mbaya iliyotokea Kijiji cha Utaho, Kata ya Puma wilayani Ikungi, Mkoa wa Singida, ikilihusisha basi lenye namba za usajili T 799 BET aina ya Nissan mali ya Kampuni ya Sumry.Ajali hiyo ilitokea juzi usiku saa 2.45 katika barabara kuu ya Singida- Dodoma umbali wa kilomita 15 kutoka Singida Mjini wakati basi hilo likitokea mkoani Kigoma kwenda jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza, Alhaji Zuberi Mbyana, anadaiwa kushindwa kuchukua hatua kwa watendaji wawili wa Mtaa wa Chamwenda, Kata ya Nyakato ambao walitoroka na fedha za wananchi.Watendaji hao; Titus Stario aliyekuwa kaimu mtendaji wa mtaa huo kati ya mwaka 2011 hadi 2013 na Dorcas Siwari aliyedumu katika wadhifa huo kwa miezi miwili mwaka 2013 kisha kutoka na fedha za wananchi sh milioni 1.5.

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, amedokeza kuwa kwa tabia na mwenendo wao, watawala wamemsaliti Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Jaji Warioba amekemea pia tabia ya watawala kumtumia Mwalimu Nyerere kama hirizi wanapotaka kupitisha mambo yao, huku wakimsaliti kwa matendo yao.

Maandamano makubwa ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Nigeria- Abuja baadaye leo watu wakiitaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwanusuru wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislam .

Mkutano wa kumi na mbili wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaaanza rasmi hii leo mjini Arusha nchini Tanzania.Miongoni mwa maswala muhimu yatakayojadiliwa ombi la Sudan Kusini kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

No comments:

Post a Comment