Pages

Wednesday, April 30, 2014

MKURUGENZI ILEMELA MATATANI

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza, Alhaji Zuberi Mbyana, anadaiwa kushindwa kuchukua hatua kwa watendaji wawili wa Mtaa wa Chamwenda, Kata ya Nyakato ambao walitoroka na fedha za wananchi.


Watendaji hao; Titus Stario aliyekuwa kaimu mtendaji wa mtaa huo kati ya mwaka 2011 hadi 2013 na Dorcas Siwari aliyedumu katika wadhifa huo kwa miezi miwili mwaka 2013 kisha kutoka na fedha za wananchi sh milioni 1.5.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Chamwenda, Lucy Kapumse na Mtendaji wa Kata ya Nyakato, Masegenghe Mathias, walithibitisha tuhuma hizo na kwamba walishamwandikia barua mkurugenzi wa manispaa ili wasakwe na kuchukulia hatua, lakini hadi sasa bado hawajakamatwa.

No comments:

Post a Comment