Ofisa Mwandamizi wa Idara ya Usalama wa
Taifa nchini, Silvanus Mzeru, ameuawa na watu wasiojulikana katika mazingira ya
kutatanisha.Mauaji hayo ambayo taarifa zake zimeibua hofu kubwa, yalitokea jana
jioni katika mataa ya barabarani karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mabweni saba ya wavulana wa Shule ya Sekondari
Ivumwe, mkoani hapa, inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM), yameteketea kwa moto na kuteketeza vifaa mbalimbali vya wanafunzi wa
shule hiyo.Moto huo ulizuka jana majira kati ya saa tatu na nne asubuhi
wakati wanafunzi hao wakiwa madarasani kuendelea na masomo yao.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama ubabe wa
madaraka na kutoelewana ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Katibu Mkuu,
Maimuna Tarishi, amepindua maamuzi ya Waziri wake, Lazaro Nyalandu na
kuwarejesha kazini vigogo wa Wanyamapori waliokuwa wameng’olewa na waziri huyo.
Maandamano na vurugu zimefanyika
leo siku ya siku ya wafanyakazi duniani katika mji mkuu wa Uturuki wa Istanbul
na maeneo mengine duniani.Maafisa wa polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi
pamoja na maji baada ya waandamanaji kukaidi marufuku ya kuandamana katika
bustani Taksim.
Rais wa Urusi, Vladmir Putin,
ametoa wito kwa Ukraine iyaondoe majeshi yake katika maeneo ya Kusini Mashariki
mwa taifa hilo na kuanza mazungumzo kama njia mojawapo ya kusuluhisha mgogoro
unaoendelea nchini humo.Ofisi ya Rais imesema kuwa wito huo ulitolewa katika
mazungumzo aliyofanya kwa njia ya simu na kiongozi wa Ujerumani, Chansela
Angela Markel.
No comments:
Post a Comment