Pages

Tuesday, April 29, 2014

MFAHAMU MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI AMONI MWAKALUKWA ANAEKUJA KWA KASI



Mwimbaji  wa nyimbo za injili Amoni Mwakalukwa  ni mzaliwa wa Mbeya wilaya ya Kyela,na ni mtoto wa kumi na moja kuzaliwa kwenye familia ya watoto kumi na mbili.Baba yake alikuwa mchungaji hivyo kumfanya akue katika mazingira mazuri sana ya kumjua Mungu .

Amoni ambaye  rasmi kabisa alianza kuimba mwaka 2008 na alifanikiwa kutoa albamu yake ya kwanza iliyoitwa “Injili ya msamaha” aliyofanya na producer Chaina Praise Studio ambayo haikufanya vizuri  sokoni.

Amesema  mwaka huu amejipanga viruri na hatimaye  kuweza kufanya albamu mpya ambayo inakwenda kwa jina la “Nitetee” akizungumza na blog ya  Maisha yetu akasema “Hivi nimejipanga vyema katika kufanya uzinduzi wa albamu yangu ya “Nitetee”utakao fanyika tarehe 8/06/2014.

Pia Amon amewashauri waimbaji wa nyimbo za injili kuendeleza mazuri  wanayoyaimba hata katika jamii akisema “Waimbaji tujitahidi kuishi kama tunavyoimba siyo tuimbe kwa kutoa ujumbe mzuri na tuishi kwa kutenda maovu.

No comments:

Post a Comment