Pages

Friday, April 17, 2015

HABARI KWA UFUPI




Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilizindua mkakati wake wa ushindi “Hakuna kulala, hakuna kula mpaka kieleweke” katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba kwa kufungua mafunzo yatakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa vyama na Serikali za Mitaa


Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imepunguza nauli za mabasi ya mikoani huku ikitangaza kubaki kama zilivyokuwa, zile za daladala baada ya ukokotoaji wake kuonyesha tofauti ndogo ya punguzo kulinganisha na viwango vya sasa.

Kumekuwa na mashambulizi zaidi usiku dhidi ya biashara zinazomilikiwa na raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mipira kutawanya umati kusini mwa mji wa Johannesburg ambapo gari na nyumba vilichomwa moto.Msemaji wa polisi aliiambia BBC kuwa karibu raia mia mbili wa kigeni walikimbilia usalama kwenye kituo cha polisi lakini wakaondoka muda baadaye.

Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limetoa kanda yenye ushahidi inayoonyesha matumizi ya gesi ya chlorine kwenye shambulizi moja mwezi uliopita nchini Syria.Kanda hiyo inaonyesha watoto watatu walio chini ya miaka minne ambao walikufa licha ya kuwepo jitihada za kuwakoa.

Viongozi wa vyama vitano vya upinzani wameshiriki katika mdahalo wa pili wa moja kwa moja ulioandaliwa na BBC.Katika hoja za kwanza, kiongozi wa chama cha Labour, Ed Miliband, amesema suala la familia za wafanyakazi atalipa kipaumbele kwanza, wakati kiongozi wa UK Independence Party,UKIP, Nigel Farage amesema atasaidia biashara ndogo ndogo.

No comments:

Post a Comment