Pages

Wednesday, July 23, 2014

FUTARI YAUA WATOTO WATATU WA FAMILIA MOJA

Watoto watatu wa familia moja wamefariki dunia baada ya kula futari inayosadikiwa kuwa na sumu katika Kijiji cha Kwasunga, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.


Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Costantine Massawe alisema tukio hilo lilitokea juzi saa tatu usiku, ambapo watoto hao wanatoka kwenye familia ya Jumbe Waziri (40).

Alisema familia hiyo ilikula futari hiyo akiwemo Waziri, wake zake wawili na watoto ambapo wote walianza kujisikia vibaya, kukimbizwa katika Kituo cha Afya kilichopo Mkata wilayani humo, lakini watoto hao walifariki dunia na wazazi wao wamelazwa hospitalini hapo.

Aliwataja watoto hao waliofariki kuwa ni Mwajuma Jumbe (3), Ramadhani Jumbe (5) na Abdi Jumbe (7),  ambapo baada ya wazazi wao kupata matibabu kituoni hapo, waliruhusiwa kutokana Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha vifo hivyo.

No comments:

Post a Comment