Pages

Wednesday, June 04, 2014

HABARI KWA UFUPI




Wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini, Kanda ya Kaskazini wamethibitisha uwepo wa hazina ya madini ya dhahabu katika Mlima Rankiroga na Mto Karabaline katika Kijiji cha Mgongo, Kata ya Samunge, Wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha.


Mbunge wa Rungwe Magharibi, Profesa Mark Mwandosya, amefanya maamuzi magumu ya kuinusuru Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuanguka bungeni.Mwandosya ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Kazi Maalumu, alifanya maamuzi hayo juzi wakati akitoa kauli ya serikali kuhusu hoja nzito ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), aliyeitaka serikali kutangaza tatizo la maji kuwa janga la kitaifa na kutangaza mpango kabambe wa kukabiliana nalo.

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, imeingia katika kashfa nzito ya kudaiwa kutafuna zaidi ya sh milioni 200 za kujenga ukuta wa kuzuia kuanguka kwa jengo la lililokuwa Shirika la Uvuvi nchini (Tafico)  kutokana na mmomonyoko unaosababishwa na maji ya bahari.

BBC imepata taarifa kuwa zaidi ya watu 20 wameuawa katika mashambulio katika vijiji vya jimbo la Borno.Hii inatokea wakati bado kuna wasiwasi mkubwa juu ya hatma ya wasichana zaidi ya 200 waliotekwa nyara na kundi hilo yapata siku 50 zilizopita.

Rais Barack Obama anatarajiwa kumteua balozi wa kwanza wa Somalia, mara ya kwanza tangu nchi hiyo itumbukie katika vita vya wenyewe kwa wenyewe zaidi ya miongo miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment