Pages

Friday, April 11, 2014

OPRAH WINFREY APATA HAKI YA KUONYESHA FILAMU YA MANDELA

Los Angeles, Marekani. Mwanamama mwenye ushawishi Duniani Opra Winfrey, kupitia Kituo chake cha runinga cha ‘OWN’, amepata haki ya kuonyesha filamu ya marehemu Mandela iitwayo ‘Long Walk to Freedom’.

Filamu hiyo imeshapata umaarufu mkubwa na kutajwa kuwania tuzo kadhaa. Itakuwa inaeleza maisha halisi ya mwanamapinduzi huyo.
Kwa mujibu wa waandaaji wa filamu hiyo, itachukua miaka mitatu kabla ya kuanza kuonyeshwa kwenye runinga na itakapoanza kituo cha kwanza kuionyesha kitakuwa ni ‘OWN’ ambacho kimenunua haki hizo kutoka kwenye Kampuni ya ‘The Weinstein’.

Miongoni mwa watu waliowahi kumfanyia mahojiano yaliyojaa kila aina ya ushujaa, vilio hayati Nelson Mandela ni mtangazaji Opra ambaye alihudhuria mazishi ya mwanamapinduzi huyo jasiri Kijijini cha Qunu, alikozaliwa Mandela. From Mwananchi

No comments:

Post a Comment