Pages

Friday, April 11, 2014

CHAI YAPUNGUZA HATARI YA KIFO


 Wanasayansi nchni China wameuamsha ulimwengu kwa mara nyingine baada ya kubaini kuwa chai ndiyo dawa kwa watu wanaotaka kuishi maisha marefu. Utafiti uliochapishwa kwenye jarida  la kimarekani la afya na maisha, ulieleza kuwa unywaji wa chai unasaidia kwa asilimia 10 kupunguza hatari ya kifo. 
Watafiti hao walionyesha kuwa kunywa chai mara kwa mara kunapunguza msongo wa mawazo, tatizo ambalo husababisha watu wengi kupoteza maisha.Hata hivyo utafiti huo ulionyesha  katika siku za karibuni sababu za vifo si hali mbaya ya kiuchumi pekee ama jinsia, umri au elimu bali ni baadhi ya tabia ikiwemo kula matunda na chai ya rangi. (green tea).

No comments:

Post a Comment