Pages

Thursday, March 13, 2014

SOMA HABARI KWA UFUPI




Wakati mataifa mbalimbali duniani yakiadhimisha siku ya Afya ya Figo Duniani leo,ugonjwa huo unaendelea kuwakumba mamilioni ya watu.Takwimu zinaonyesha kuwa,mwanaume mmoja kati ya watano,na mwanamke mmojakati ya wanne walio na umri kati ya miaka 65 na 74 wanaugonjwa sugu wa Figo.
                   *************************
Ndege wa ajabu wanaosadikiwa kutoa kinyesi chenye sumu kali,wamevamia kisiwa cha musira kilichopo Manispaa ya Bukoba na kusababisha vifo vya mifugo kama ndege  anaofugwa,huku ukali wa sumu hiyo ukisababisha kutoboka mabati ya nyumba zilizopo kisiwani humo.
                        **************************
Serikali ya Uchina imechapisha picha zilizonaswa na mtambo wake wa satelite zikionyesha mabaki ya kitu kipana kikielea katika bahari ya Kusini mwa Uchina.
Picha hizo zilipigwa siku ya Jumapili, saa ishirini na nne baada ya ndege ya abiria ya Malaysia kutoweka ikiwa na abiria 239, lakini haijabainika ikiwa vifaa hivyo ni vya ndege hiyo.
                        ***************************
Rais wa Marekani Barrack Obama, ameonya Urussi kusitisha mpango wake wa kutaka kutwaa eneo la Crimea nchini Ukraine lasivyo iwekewe vikwazo.

No comments:

Post a Comment