Pages

Wednesday, June 11, 2014

UNYAMA HUU MPAKA LINI "FAMILIA YAUAWA KWA KUKATWAKATWA NA MAPANGA"


Watu watatu wa familia moja, akiwemo mwanafunzi wa sekondari, wameuawa kinyama kwa kukatwa mapanga shingoni na sehemu mbalimbali za miili yao na watu wasiojulikana.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alisema tukio hilo limetokea juzi saa 2:30 usiku katika Kijiji cha Msungua, Kata ya Irisya, Tarafa ya Sepuka wilayani Ikungi wakati wanafamilia hao wakiwa wamelala ndani.

Alisema kuwa marehemu hao waligundulika baada ya majirani kuona mwili wa mwanamke ukiwa nje, ndipo walianza kutaharuki na walipofuatilia ndani walikuta mwili wa mwanaume ukiwa umelezwa kitandani.
Aliwataja marehemu hao kuwa ni Mussa Mkuki (92), mkewe Tatu Sefu (69) na mwanafunzi wa Shule ya 

Sekondari Gumanga wilayani Mkalama, Jasmin Idd (17) ambaye alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika zahanati ya Kijiji cha Sepuka.
Kamanda Kamwela alisema kuwa pia mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Kisuluda, Mussa 
Nasoro, alijeruhiwa vibaya na kulazwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida huku hali yake ikielezwa kuwa  mbaya.

Uchunguzi wa daktari umebaini kuwa watu hao walipoteza maisha kutokana na kuvuja damu nyingi katika majeraha waliyoyapata.

Hadi sasa chanzo cha tukio hilo la kutisha hakijafahamika na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wake wa kina ili kubaini waliohusika.Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment